Uamuzi huo ulitangazwa jana na
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kamati hiyo kukutana na maofisa
wa BoT na kupokea maelezo kuhusu Sh201 bilioni za akaunti ya Escrow na
mazingira ya kuchukuliwa kwake.
Fedha hizo ziliwekwa katika akaunti hiyo na wadau, Tanesco na IPTL baada ya kuibuka mgogoro wa kisheria kutokana na madai kuwa shirika hilo la umeme lilikuwa linalipa gharama kubwa za uwekezaji zaidi ya makubaliano.
Iliamuriwa fedha hizo zihifadhiwe hadi mgogoro utakapokwisha, lakini fedha hizo zikachukuliwa na kampuni iliyonunua IPTL, Pan African Power Solution (PAP).
Mbali na CAG, PAC pia imeagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ianze uchunguzi wa mchakato mzima wa mkataba wa IPTL, umiliki wa kampuni hiyo na uhamishaji wa umiliki kwenda kampuni ya PAP.
"Kamati imeagiza ukaguzi maalumu kutoka PAC ili kupata ukweli. PAC imetoa mpaka mwisho wa mwezi ujao taarifa ya ukaguzi huo iwe imekamilika na kuwataka wahusika wote wa mchakato wa IPTL kusubiri matokeo ya ukaguzi," alisema Zitto na kuongeza: "PAC imetaka pia uamuzi wa mahakama kuheshimiwa."(E.L)
Fedha hizo ziliwekwa katika akaunti hiyo na wadau, Tanesco na IPTL baada ya kuibuka mgogoro wa kisheria kutokana na madai kuwa shirika hilo la umeme lilikuwa linalipa gharama kubwa za uwekezaji zaidi ya makubaliano.
Iliamuriwa fedha hizo zihifadhiwe hadi mgogoro utakapokwisha, lakini fedha hizo zikachukuliwa na kampuni iliyonunua IPTL, Pan African Power Solution (PAP).
Mbali na CAG, PAC pia imeagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ianze uchunguzi wa mchakato mzima wa mkataba wa IPTL, umiliki wa kampuni hiyo na uhamishaji wa umiliki kwenda kampuni ya PAP.
"Kamati imeagiza ukaguzi maalumu kutoka PAC ili kupata ukweli. PAC imetoa mpaka mwisho wa mwezi ujao taarifa ya ukaguzi huo iwe imekamilika na kuwataka wahusika wote wa mchakato wa IPTL kusubiri matokeo ya ukaguzi," alisema Zitto na kuongeza: "PAC imetaka pia uamuzi wa mahakama kuheshimiwa."(E.L)
0 comments: