Thursday, 25 August 2016
Tuesday, 23 August 2016
Mpiga tarumbeta
Headley Bennett, ambaye alishiriki katika wimbo wa kwanza wa mwanamuziki
maarufu wa nyimbo za rege Bob Marley 'Judge Not,' amefariki akiwa na
umri wa miaka 85.
Mwanawe Carol Bennett, alithibitisha kifo cha mwanamuziki huyo siku ya Jumapili.Carol hakusema sababu maalum ya kifo cha mwanamuziki huyo, lakini alisema babake alikuwa akiugua shinikizo la damu na hivi majusi alipatika na saratani ya kiume.
Alituzwa na serikali ya Jamaica mwaka wa 2005 kama Mjamaica wa sita mwenye hadhi ya juu.
Moja
ya headline kwenye mitandao ya kijamii iliyochukua nafasi usiku wa
August 22 2016 ni pamoja na tukio la kumbukumbu ya kuzaliwa kwa staa wa
bongo flava kutokea katika label ya WCB Raymond ambapo uongozi wake uliamua kumfanyia suprise ya zawadi ya gari aina ya Toyota Rav 4 yenye thamani ya milioni 20 za kitanzania.
Leo August 23 Raymond kupitia ukurasa wake wa instagram aliamua kuyatoa yake ya moyoni kwa kuandika…>>>’Kweli
Nimeamini Mungu Hana upendeleo.nilikua mtu nilie jikatia tamaa ndani ya
miaka takribani mi nne nilikua nikiangaika na muziki wangu nakushukuru
sana sana‘
‘Kaka Lao Diamond Platnumz Umenifundisha vitu vingi saaaaaanaaa hadi leo naiona njia boss wangu Babu Tale ni mwaka wa tano sasa toka Umenijua umenivumilia kwa mengi hadi leo hii haujanichoka na unanisaidia kwa moyo mmoja’
‘Boss Sallam Sk Asante sana kwakupigania kila siku thamani ya muziki wangu nakuakikisha nafika sehemu nzuri Mkubwa Fella wewe ni zaidi ya mzazi maana umenilea nakunifundisha meeengi kwenye muziki‘
‘Madee Sitoacha kukushukuru kaka lao wewe nikioo naamini unafurahi kuniona mdogo wako hapa nilipo maana unanijua saaaaanaaaa‘
Thursday, 14 July 2016
Wimbo wa mapenzi
wa mwanamuziki wa Uingereza Ed Sheeran unaongoza kwa kupendwa sana na
watu kama wimbo wa kufungua jukwaa wakati wa harusi.
Kwa mujibu wa
mtandao wa Spotify, ambao wamechunguza maelfu ya orodha ya nyimbo
zinazosambazwa zaidi katika mtandao huo, wimbo wa Thinking Out Loud
unaongoza.Wimbo wa At Last wake Etta James ni wa pili nao wimbo wa Ray LaMontagne, You Are the Best Thing ni wa tatu.
Nyimbo nyingine maarufu zilizo kwenye orodha ya 50 bora duniani ni wimbo wake Frank Sinatra uitwao The Way You Look Tonight na wimbo wa Marry You wake Bruno Mars.
- Thinking Out Loud - Ed Sheeran
- At Last - Etta James
- You Are the Best Thing - Ray LaMontagne
- All of Me - John Legend
- A Thousand Years - Christina Perri
- Make You Feel My Love - Adele
- I Won’t Give Up - Jason Mraz
- Everything - Michael Bublé
- Better Together - Jack Johnson
- Amazed - Lonestar
Taarifa kutoka katika Magazeti ya Udaku na Blogs kadhaa mjini zinaeleza kuwa Polisi wenye Silaha hivi karibuni walifika Nyumbani kwa msanii Diamond Plutnumz na kuzima Shughuli iliyokuwa ikiendelea.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, shughuli iliyositishwa na polisi ilikuwa ni ile ya kusherehekea siku ya kuzaliwa ya mama mzazi wa mkali huyo wa muziki, Sanura Kassim ‘Sandra’ iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Ilidaiwa kwamba msanii huyo amekuwa akifanya sherehe mara kwa mara katika nyumba yake hiyo, hali inayosababisha kero kwa baadhi ya majirani zake, ambao nao, wamekuwa wakilalamika mara kwa mara kwa viongozi wa serikali ya mtaa huo.
Gazeti hili baada ya kuupata ubuyu huo, lilifunga safari hadi nyumbani kwa msanii huyo na ku kia ofisini kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mivumoni, Deodatus Kamugisha ambaye baada ya kuulizwa kuhusu kuwepo kwa tukio hilo la askari kuzima sherehe hiyo, alikiri kuwa ni kweli.
“Nimekuwa nikipata malalamiko ya mara kwa mara kuhusu sherehe za Diamond kuwa waalikwa wake ni vijana wa kihuni ambao wakija huwa wanavuta bangi hadharani, wanafunga barabara pamoja na kujisaidia haja ndogo hovyohovyo maeneo ya nje ya nyumba yake.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mivumoni, Deodatus Kamugisha.
“Juzi nilipigiwa simu usiku na majirani zaidi ya sita wakila lamika kuhusu sauti kubwa ya muziki wa kwenye sherehe ya Diamond, nilimuita lakini akakaidi, ikabidi niende Kituo cha Polisi cha Wazo na kuchukua polisi wakiwa na silaha na kwenda kufunga sherehe ile, sheria iko wazi kuhusu utaratibu wa kupiga muziki maeneo ya baa na majumbani,” alisema Kamugisha.
Baadhi ya majirani waliozungumza na gazeti hili, walisema kumekuwa na tabia ya Diamond kufanya sherehe mara kwa mara nyumbani hapo, huku muziki mkubwa ukipigwa, jambo ambalo kwao ni kero.
“Nachukizwa sana na kelele za Diamond, kwani watu tunashindwa kulala kwa sababu yeye anafanya sherehe mbona kuna kumbi na hoteli anaweza kwenda tu, mimi nyumba yangu ni kama kilomita mbili kutoka kwake, lakini nasikia muziki kwa kero, je walio ubavuni mwake si wanataabika sana!” alisema mzee mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Gazeti hili lilimtafuta Diamond kwa simu yake mkononi ili kuzungumzia ishu hiyo lakini iliita bila kupokelewa kwa muda wote.
Thursday, 30 June 2016
Monday, 9 May 2016
Tuesday, 3 May 2016
SAD NEWS..!! Afeni Shakur Davis,mama mzazi wa
the late Tupac Shakur amefariki dunia akiwa na miaka 69,kwa mujibu wa
maafisa wa polisi wa Sausalto,California wamedai kuwa Afeni alifariki
dunia usiku wa kuamkia leo akiwahishwa hospitali mara baada ya kupata
taarifa ya simu ya dharura kutoka nyumbani kwake.
Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi inayoeleza chanzo cha kifo chake,so lets wait and see.
Afeni Shakur.
Tupac ambae ni miongoni mwa rappers
wanaoheshimika na jamii ya wanamuziki wa HipHop Ulimwenguni alipigwa
risasi September 7 1996 jijini Las Vegas,Nevada na kufariki baada ya
siku 6 akiwa na umri wa miaka 25.

Picha hizi zimeleta wasiwasi kuwa huenda wawili hao walikuwa pamoja wakiogelea huku wengine wakimtetea Zari na kusema kuwa yeye alikuwa hiyo sehemu...
siku nyingi lakini Ivan ameenda sehemu hiyo hiyo na kupiga picha na kuzitupia mtandaoni leo kumuumiza Diamod na kuwapa watu cha kuongea.
Kesi ya Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
‘TRA’, Harry Kitilya, Sioi Solomoni na aliyekuwa afisa mwandamizi benki
ya Stanibic tawi la Tanzania pia ni Miss Tanzania 1996, Shose Sinare.

Kesi hiyo ilitajwa kusikilizwa leo May 3 2016 Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam ambapo imehailishwa tena hadi Mei 18 2016 kutokana na Jalada la kesi hiyo ambalo lilitegemewa kurudi leo lakini halijarudi na watuhumiwa wamerudishwa tena rumande.
Aidha watuhumiwa walitakiwa kufika mahakama Kuu kwa ajili ya kuendelea na rufani ambapo baada ya kufika Mahakama Kuu kanda ya Dar es salaam imepanga kuanza kusikiliza rufani hiyo May 5 2016.
Kesi hiyo ilitajwa kusikilizwa leo May 3 2016 Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam ambapo imehailishwa tena hadi Mei 18 2016 kutokana na Jalada la kesi hiyo ambalo lilitegemewa kurudi leo lakini halijarudi na watuhumiwa wamerudishwa tena rumande.
Aidha watuhumiwa walitakiwa kufika mahakama Kuu kwa ajili ya kuendelea na rufani ambapo baada ya kufika Mahakama Kuu kanda ya Dar es salaam imepanga kuanza kusikiliza rufani hiyo May 5 2016.
Msanii wa kundi la Navy Kenzo, Aika, amefunguka na
kuzungumzia faida ya tour yao ya ‘Kamatia Chini Tour’ ambayo ilifanyika
katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.

Akizungumza na Bongo5 Ijumaa hii, Aika amesema tour hiyo iliwasaidia kuwatangaza kwani walikutana na mashabiki wao ambao walikuwa hawaamini kama wao ndio wameimbi wimbo ‘Kamatia Chini’.
“Kuna vitu vingi kama wasanii tumejifunza, next time ili tujirekebishe na kusawazisha makosa yetu na kufanya kitu kikubwa zaidi,” alisema Aika.
“Mapokezi ya ‘Kamatia Chini’ mkoani yalikuwa makubwa sana isitoshe wimbo ulikuwa hata haijafikisha wiki 2, lakini kila mtu alikuwa anaimba, yaani watu walivyosikia wale watu waliyoimba ‘Kamatia Chini’ wamefika, wengine walikuwa wanakataa. Wanasema hawawezi kuwa hawa, lakini sisi tukawaonyesha sisi ni Watanzania na ndiye tuliyoimba ule wimbo,” aliongeza Aika.
Akizungumza na Bongo5 Ijumaa hii, Aika amesema tour hiyo iliwasaidia kuwatangaza kwani walikutana na mashabiki wao ambao walikuwa hawaamini kama wao ndio wameimbi wimbo ‘Kamatia Chini’.
“Kuna vitu vingi kama wasanii tumejifunza, next time ili tujirekebishe na kusawazisha makosa yetu na kufanya kitu kikubwa zaidi,” alisema Aika.
“Mapokezi ya ‘Kamatia Chini’ mkoani yalikuwa makubwa sana isitoshe wimbo ulikuwa hata haijafikisha wiki 2, lakini kila mtu alikuwa anaimba, yaani watu walivyosikia wale watu waliyoimba ‘Kamatia Chini’ wamefika, wengine walikuwa wanakataa. Wanasema hawawezi kuwa hawa, lakini sisi tukawaonyesha sisi ni Watanzania na ndiye tuliyoimba ule wimbo,” aliongeza Aika.
Monday, 2 May 2016
Sunday, 1 May 2016
Mume wa Tiwa Savage, Tee Billz alipost mfululizo wa malalamiko kwenye Instagram kuhusu kumtuhumu mke wake kuwa alimsaliti na Doj Jazzy, Dr Sid na 2Face Idibia.

Jamaa huyo alionesha nia ya kutaka kujiua kutokana na masahibu hayo. Hiyo ilipelekea jamii kubwa ya Nigeria imchukie Tiwa kwa kumuona kama mwanamke katili na anayemtesa mumewe. Lakini upande wa pili wa shilingi wa mkasa huo unaweza ukabadili mawazo yako.
Kwa mujibu wa Tiwa, mume wake ndiye mzinguaji mkubwa na ana vimbwanga haswaa.
Akiongea kwenye exclusive interview na Pulse TV, Tiwa alisimulia jinsi ambavyo mume wake alikuwa akimfanyia ikiwa pamoja na kumtelekeza kwa kutotaka kujua chochote pale alipolazwa hospitali nchini Jamaica alikoenda kufanya video na Busy Signal.
Anasema wakati anajiandaa kwenda kushoot, alianza kutoka damu nyingi ukeni kiasi cha kupoteza fahamu. Alimpigia simu na kumtumia ujumbe mumewe ikiwa pamoja na kumtumia picha akiwa hoi kitandani lakini hakujibiwa hadi anatoka hospitali.
Siku amerejea Nigeria na akiwa amelala usiku wa saa nane, simu ya mumewe iliita kwa namba iliyohifadhiwa kwa jina la biashara lakini alishangaa iweje kampuni impigie usiku huo. Anadai alichukua simu ya mumewe na kuanza kusoma ujumbe wa WhatsApp na ndipo alipogundua kuwa huyo alikuwa ni mwanamke na maongezi yao yalionesha kuwa walikutana hotelini na kufanya mapenzi. Kutokana na kitendo hicho aliondoka na kwenda kwa rafiki yake.
Anadai kuwa amekuwa akificha kwa muda mrefu kuhusu mume wake, lakini amedai tangu mtoto wao azaliwa, hajawahi kutumia hata senti kwaajili ya familia yao kwamba Tiwa ndiye kila kitu.
Amesimulia pia jinsi ambavyo mume wake amekuwa na tabia ya kumzunguka kwenye malipo ya show zake ambapo ametolea mfano wa harusi aliyotakiwa kwenda kutumbuiza London. Anasema alibaini kuwa mumewe alilipwa gharama zote lakini hadi anaenda kutumbuiza alimueleza kuwa hakuwa amelipwa. Kwakuwa alikuwa anafahamiana na miongoni mwa waandaji wa harusi hiyo alimuuliza na kujibiwa kuwa walikuwa wameshamlipa mume wake hela yote, miezi minne nyuma.
“Unamuibia mke wako, na yeye haoni kama ameniibia mimi, kwahiyo ilibidi nitumbuize kwenye harusi bure, kwasababu alikuwa ameshatapeli hela na sijui alizifanyia nini,” anasimulia.
Kwa upande mwingine staa huyo alieleza jinsi ambavyo mume wake alikuwa akiishia maisha ya zaidi ya kipato chake na hivyo wakati mwingine kumfanya ajikute kwenye madeni makubwa ambayo alilazimika kuyalipa.
Tiwa anasema jambo ambalo mume wake alizingua zaidi na ambalo limesababisha mgogoro wao ni pale alikopa naira milioni 45 ambazo ni sawa na shilingi milioni 495 za Kitanzania na kuchikichia. Kwa hali hiyo Tiwa alianza kuhofia usalama wake kwamba wanaomdai mumewe wangeweza hata kumdhuru ama kumteka yeye na mwanae kwasababu ya deni hilo.
Pia Tiwa amezungumzia jinsi ambavyo aligundua mume wake anatumia cocaine kitu ambacho kilimuumiza sana.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo alikanusha kwa msisitizo kuwa hajawahi kamwe kumsaliti mume wake na Don Jazzy, Dr Sid wala 2Face na kwamba yupo tayari hata kuwekewa kifaa cha kubaini kama anasema uongo.
Mpaka hapo Tiwa ameonesha nia ya kuachana na mume wake, kitu ambacho anadai hakupenda kiwe.
Jamaa huyo alionesha nia ya kutaka kujiua kutokana na masahibu hayo. Hiyo ilipelekea jamii kubwa ya Nigeria imchukie Tiwa kwa kumuona kama mwanamke katili na anayemtesa mumewe. Lakini upande wa pili wa shilingi wa mkasa huo unaweza ukabadili mawazo yako.
Kwa mujibu wa Tiwa, mume wake ndiye mzinguaji mkubwa na ana vimbwanga haswaa.
Akiongea kwenye exclusive interview na Pulse TV, Tiwa alisimulia jinsi ambavyo mume wake alikuwa akimfanyia ikiwa pamoja na kumtelekeza kwa kutotaka kujua chochote pale alipolazwa hospitali nchini Jamaica alikoenda kufanya video na Busy Signal.
Anasema wakati anajiandaa kwenda kushoot, alianza kutoka damu nyingi ukeni kiasi cha kupoteza fahamu. Alimpigia simu na kumtumia ujumbe mumewe ikiwa pamoja na kumtumia picha akiwa hoi kitandani lakini hakujibiwa hadi anatoka hospitali.
Siku amerejea Nigeria na akiwa amelala usiku wa saa nane, simu ya mumewe iliita kwa namba iliyohifadhiwa kwa jina la biashara lakini alishangaa iweje kampuni impigie usiku huo. Anadai alichukua simu ya mumewe na kuanza kusoma ujumbe wa WhatsApp na ndipo alipogundua kuwa huyo alikuwa ni mwanamke na maongezi yao yalionesha kuwa walikutana hotelini na kufanya mapenzi. Kutokana na kitendo hicho aliondoka na kwenda kwa rafiki yake.
Anadai kuwa amekuwa akificha kwa muda mrefu kuhusu mume wake, lakini amedai tangu mtoto wao azaliwa, hajawahi kutumia hata senti kwaajili ya familia yao kwamba Tiwa ndiye kila kitu.
Amesimulia pia jinsi ambavyo mume wake amekuwa na tabia ya kumzunguka kwenye malipo ya show zake ambapo ametolea mfano wa harusi aliyotakiwa kwenda kutumbuiza London. Anasema alibaini kuwa mumewe alilipwa gharama zote lakini hadi anaenda kutumbuiza alimueleza kuwa hakuwa amelipwa. Kwakuwa alikuwa anafahamiana na miongoni mwa waandaji wa harusi hiyo alimuuliza na kujibiwa kuwa walikuwa wameshamlipa mume wake hela yote, miezi minne nyuma.
“Unamuibia mke wako, na yeye haoni kama ameniibia mimi, kwahiyo ilibidi nitumbuize kwenye harusi bure, kwasababu alikuwa ameshatapeli hela na sijui alizifanyia nini,” anasimulia.
Kwa upande mwingine staa huyo alieleza jinsi ambavyo mume wake alikuwa akiishia maisha ya zaidi ya kipato chake na hivyo wakati mwingine kumfanya ajikute kwenye madeni makubwa ambayo alilazimika kuyalipa.
Tiwa anasema jambo ambalo mume wake alizingua zaidi na ambalo limesababisha mgogoro wao ni pale alikopa naira milioni 45 ambazo ni sawa na shilingi milioni 495 za Kitanzania na kuchikichia. Kwa hali hiyo Tiwa alianza kuhofia usalama wake kwamba wanaomdai mumewe wangeweza hata kumdhuru ama kumteka yeye na mwanae kwasababu ya deni hilo.
Pia Tiwa amezungumzia jinsi ambavyo aligundua mume wake anatumia cocaine kitu ambacho kilimuumiza sana.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo alikanusha kwa msisitizo kuwa hajawahi kamwe kumsaliti mume wake na Don Jazzy, Dr Sid wala 2Face na kwamba yupo tayari hata kuwekewa kifaa cha kubaini kama anasema uongo.
Mpaka hapo Tiwa ameonesha nia ya kuachana na mume wake, kitu ambacho anadai hakupenda kiwe.