Thursday, 25 August 2016

Mwanamume  abeba maiti ya mkewe 12km

Amang Majhi alifariki dunia kwa maradhi ya kifua kikuu Jumanne usiku
Mwanamume mmoja maskini nchini India alibebe maiti ya mkewe kwa zaidi ya kilomita 12 baada ya hospitali alimofariki kushindwa kumsafirisha kwa gari la kuwabebea wagonjwa hadi kijiji mwake.
Mke wa Dana Mjhi, Amang, mwenye umri wa 42, alifariki dunia baada ya kuugua maradhi ya kifua kikuu katika hospitali ya Ulaya, mji wa Bhawanipatna jimbo la Orissa.
Bwana Mahji alisema kijiji chake kilikuwa umbali wa kilimita 60 na hakuwa na uwezo wa kulipa gharama ya usafiri wa gari la kuwabebea wagonjwa.
Hospitali hiyo imekana madai hayo.

'Hakuna namna'

'Mwanamke huyo alilazwa hospitalini siku ya Jumanne na kufariki usiku huo huo.
Bwana yake alichukua maiti hiyo bila kuwafahamisha wahudumu wa hospitali hiyo,' afisa mkuu wa afya B Brahma alisema
Bwana Majhi, anadai mkewe alifariki siku ya Juma nne usiku na kuamua kubeba mwili wake siku ya Jumatano baada ya wahudumu wa hospitali hiyo kumsihi kuondoa mwili huo.
' Nilikuwa nikiwaomba wahudumu wa hospitali hiyo wanisaidie gari nimbebe mke wangu lakini nikaambulia patupu.
Kwa sababu mimi ni maskini na nisingeweza kukodisha gari la kibinafsi sikuwa na njia nyingine ila kumbeba mke wangu mabegani.'

Wakati akitembea , Bw Majhi alisindikizwa na mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 12 , Chaula
Mapema Jumatano , alisema alifunga mwili wa mkewe na nguo na kuanza safari hiyo ndefu ya kuelekea kijijini huko Melghar kwa mila na tamanduni za mwisho akiungana na mwanawe mwenye umri wa miaka 12 , Chaula.
Alitembea kwa takriban kilomita 12, ndipo watu walipoingilia kati na kumsaidia kwa gari la kubebea wagonjwa wakamfikisha hadi mwisho wa safari yake.
Shughuli ya kuchoma mwili wa mkewe ilifanyika siku ya Jumatano usiku

Thursday, 14 July 2016

Shambulio laua watu zaidi ya 80 Ufaransa

Zaidi ya watu 80 wameripotiwa kuuawa katika shambulio lililotokea katika mji wa Nice kusini mwa Ufaransa.
Lori lililokuwa likienda mwendo kasi lilijiingiza katika mkusanyiko wa watu waliokuwa wakiangalia maonesho ya fataki kuadhimisha siku ya kitaifa ya Bastille, ambayo huja na shamra shamra kila mwaka.
Mwendesha mashtaka katika mji wa Nice, Jean- Michel Pretre amesema lori hilo liliendelea kutembea kilo mita mbili kabla ya polisi kumpiga risasi dereva.

Rais Francois Hollande amerudi mjini Paris kwa ajili ya kufanya kikao cha dharura.
Hali ya tahadhari iliyowekwa toka kutokea kwa shambulio lililofanywa na Islamic State mjini Paris, bado iko palepale nchini Ufaransa.
Huyu ndiye Kuku Ghari zaidi Duniani, Jogoo anauzwa kwa Dola 2000 za Kimarekani.


Basi unaambiwa kuwa hii ndiyo aina ya Kuku mwenye gharama kubwa zaidi Duniani.. Ukihitaji Jogoo mmojawapo aliyekomaa ili umfuge basi itabidi uwe na $2000., Na sababu kuwa ni kwa sababu wapo wachache mno.
Kuku hawa wanafahamika kama ‘Ayam Cemani’ chimbuko lao ni kule Indonesia, unaambiwa kila kitu kwenye Mwili wao ni cheusi, kuanzia ngozi, maini, utumbo, macho, moyo, ubongo, kiini cha yai lake, nyama yenyewe mpaka kinyesi chao…
Sababu ya weusi huu ni kutokana na wingi wa Melanin kwenye seli zao na hali hii kijenetiki hufahamika “fibromelanosis”.
Raia wa Uganda waweka picha za utani mitandaoni baada ya Rais Museveni kuongea na simu pembeni ya barabara

Jana Julai 12 Rais wa Uganda, Yoweri Museveni alisimamisha msafara wake na kuketi pembezoni mwa barabara ambapo alizungumza na simu kwa takribani dakika 30.
Baada ya raia wa nchi hiyo kuona kitendo hicho, nao walianza kuweka picha kwenye mitandao ya kijamii wakiwa wanaongea na simu pembezoni mwa barabara na wengine ku-edit picha ya Rais Museveni na kuiweka maeneo tofauti tofauti
Hapa chini ni picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii.
- -- --- ---- ----- ------ ------- -------- 1 (1) 2 (1) 2 (2) 11 12 13 14 15 16

M72 M73 M74 m76

Wednesday, 13 July 2016

Unyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti
Ripoti mpya inasema watoto wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.
Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pediatrics, huo ni ni usafi dhanio,kwani yatokanayo na baadhi ya wadudu huimarisha mfumo wa kinga ya mwili.
Unyonyaji wa kidole gumba na ung’ataji wa kucha umeonekana kuzuia baadhi ya alergy.
Kati ya watu elfu moja wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi thelathini na mbili,walifanyiwa uchunguzi kwa muda nchini New Zealand.
Lakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Uchunguzi uliofanywa na kurekodiwa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano na kumi na moja na wengine waliofanyiwa vipimo ni wenye umri kati ya miaka kumi na tatu na thelathini na miwili.
Huku thuluthi moja ya watoto hao ni wanyonyaji wa vidole mara kwa mara au hung’ata kucha zao na katika vipimo walivyofanyiwa watoto hao wameonekana kuwa wana kiwango kidogo cha kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.

Watoto wanaoweza kupata matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani (alergy) kutokana na vitu kama vumbi kutoka majumbani,manyoya ya paka au mbwa, lakini watoto wenye kunyonya vidole gumba na kung’ata kucha walikuwa ni chini ya theluthi moja kuliko watoto wenye tabia hii ya unyonywaji vidole.
Na tabia hii ya unyonyaji vidole au ung’ataji kucha inaonekana kuwa kinga mpaka wanapofikia umri wa utu uzima.
" kuwa na paka au mbwa majumbani,ndugu au jamaa wanaofanya kazi mashambani pia imeonekana kuwa ni sababu kubwa inayosababisha mazingira ya ukuaji wa magonjwa yanayosababishwa na
kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.

Thursday, 21 April 2016

Director wa filamu za James Bond afariki akiwa na umri wa miaka 93


Muongazaji wa filamu ya James Bond Guy Hamilton amefariki akiwa na umri wa miaka 93.
Aliyekuwa nyota wa filamu hiyo ya 007 Roger Moore alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba alihuzunishwa na kifo chake.
160421152808__guy_hamilton_640x360_afp_nocredit
Guy Hamilton
Hamilton alimuelekeza Roger Moore katika filamu ya Live and Let Die pamoja na The man with the Golden Gun.
Pia alifanya uelekezaji katika filamu za Sean Connery in GoldFinger na Diamond are Forever.
1606
Hospitali moja katika kisiwa cha Uhispania cha Majorca ,ambapo Hamilton aliishi ilithibitisha kwa chombo cha habari cha AP kwamba amefariki sikju ya Jumatano.
Filamu nyengine zilizoelekezwa na Hamilton ni pamoja na The Battle in Britain,Force 10 from Navarone,Evil under the sun na The Mirror Crack’d.
Source: BBC & theguardian