Habari zilidai kwamba kabla ya kugeukia masumbwi, wanandoa hao walikuwa kwenye ‘pub’ yao iitwayo Milano iliyopo maeneo hayo wakijiachia kwa raha zao.
Ilisemekana kwamba Salima aliwahi kuwa mfanyakazi katika pub yao ambapo Pamela alimtuhumu kuwa na uhusiano na mumewe.
Ilidaiwa kuwa baada ya kuona simu hiyo, Pamela alimuamsha mumewe ambaye alipokea simu hiyo na kuanza kujikanyaga na kukata simu ndipo alipompigia kwa namba yake na kuanza kujibizana huku akipokea maneno ya karaha bila kutegemea mazungumzo hayo yalimtia hasira Pamela ambaye alimuuliza kwa hasira mumewe huku akitaka kujua kuna nini kati yake na huyo Salima.
Ilisemekana kuwa kelele za kipigo hicho kiliwashtua majirani ambao walisogea kwenye nyumba hiyo ili kujua nini kinaendelea na kumkuta Pamela akiwa amezimia jambo lililowafanya kutafuta msaada wa kumpeleka hospitali ili kuokoa maisha yake.
Baada ya kumfikisha dispensari walikataliwa kutokana na hali ya Pamela kuwa mbaya hivyo wakamkimbiza kwenye zahanati inayoitwa Jeshi, napo walishauri mgonjwa huyo apelekwe Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.
Pamela alifikishwa Muhimbili alfajiri ya saa 12:00 akiwa anatapika damu katika hodi ya Mwaisela na kuanza matibabu kisha kutoa taarifa katika Kituo cha Sitaki-Shari na kufunguliwa jalada la kesi namba STK/RB/70220/2014- SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI.
Habari kutoka kwa mmoja wa ndugu wa Pamela zilieleza kuwa kulitokea mvutano mkubwa wa pande mbili ambapo Alex alitaka mke arudishwe nyumbani na kuendelea na matibabu jambo ambalo lilipingwa vikali na kaka wa Pamela akisema dada yake bado ana hali mbaya.
Akizungumza kwa tabu hospitalini hapo, Pamela alikiri kufanyiwa ukatili huo na mumewe.
0 comments: